Je Kumvua Mwanamke na Kumwacha ni Sahihi?

Leave a Comment
We mwanaume mwenzangu jaribu kufikiri Mara mbili kabla ya kufanya jambo hili.

Umetumia zaidi ya mwaka mmoja kuomba mahusiano kwa mwanamke(kutongoza). Alafu baada ya kumvua nguo tu basi unakata mawasiliano apoapo hauoni ni ukatili wa kijinsia au utapeli.

Kinachonishangaza zaidi watu wenye tabia hii wanabidii kwenye kutongoza kuliko wale wanatafuta mke wa kuoa.
Ingawa inawezekana ikawa si jambo zito kwa mwanaume lakini kwa mwanamke ni majeraha makubwa moyon unayomwachia.

Unamsababishia maswali mengi kichwani kwa mfano:-
1. Labda sijui mapenzi
2. Ameniona changudoa
3.shepu yangu mbaya.

Lakini kubwa zaidi ni kwamba unasababisha ugumu kwa mwanaume atakayejitokeza kwa malengo ya kutaka kumuoa. Hataweza kutofautisha muoaji na mfunuaji.

Interview inakua ndefu  na ya mda mrefu kwa mwanaume wa kweli atakapotokea, mpaka wakati mwingine mwanaume anashindwa kwa vigezo avyopewa.

Kwakweli kama hauna malengo na mtu usimpitie na kumwacha, mnatupa shida sisi waoaji.
Next PostNewer Post Previous PostOlder Post Home

0 comments:

Post a Comment