Meet The Author

I'm a Skilled Blogger, web Developer And Creating new things as a web Designer.

author

Anthony Martial atua Manchester United kwa pauni milioni 36

Leave a Comment
Mshambuliaji kinda wa Monaco Anthony Martial amepewa ruhusa na Shirikisho la Soka la Ufaransa kuachana na majukumu ya mechi za kimataifa na kwenda England kukamilisha usajili wake Manchester United. Dili hilo la pauni milioni 36 ambalo ukichanganya na marupurupu litafika pauni milioni 58, litamshuhudia kinda huyo wa miaka 19 akipishana na Javier Hernandez aliyeuzwa Bayer Leverkusen kwa pauni milioni 12.

Taarifa ya Shirikisho la Soka la Ufaransa limesema: "Anthony Martial aliomba ruhusa kwa kocha wa timu ya taifa Didier Deschamps ili aende England kusaini mkataba na Manchester United. "Kocha alimpa ruhusa na akaondoka kwenye kambi ya timu ya taifa saa 6 mchana na atarejea Jumanne."

Martial atakuwa kinda ghali zaidi katika historia, akivunja rekodi iliyowekwa na Manchester United wakati wanamnunua beki Luke Shaw. Ataunda 'Top Three' ya makinda ghali iliyowekwa na Manchester United hiyo ikiwa ni pamoja na Wayne Rooney aliyesajiliwa na kwa pauni milioni 30 miaka 11 iliyopita.

kinda Anthony Martial ameigharimu Manchester United pauni milioni 36
Anthony Martial (kulia) anatarajia kujiunga na Manchester United kabla dirisha halijafungwa

Read More

picha: diamond akijiachia na zari

Leave a Comment

Read More

Kajala: Simruhusu Mwanangu Awe na Simu

Leave a Comment
Staa wa Sinema za Kibongo, Kajala Masanja amesema hawezi kumruhusu binti yake Paula kumiliki simu ya mkoni kwasasa.

Akiongea kwenye kipindi cha The Sporah Show hivi karibuni, Kajala alisema anaweza kufikiria kumruhusu kuwa na simu hadi pale atakapomaliza kidato cha nne.

Kajala alisema mtoto wake pia hayupo kwenye mtandao picha wa Instagram.
“Paula hana simu kabisa, sio tu simu ya Instagram hata tu kitochi, hana simu,” alisema.
“Na hawezi kuwa na simu labda mpaka afike form four, yaani nitakayomnunulia mimi,”Kajala alisisistiza.

Hongera sana Kajala kwa msimamo wako,simu ni chanzo cha maovu mengi kwa mabinti wa shule

chanzo:Bongo5
Read More

Mwenyekiti wa CCM Akutwa na Viungo vya Albino

Leave a Comment
Jeshi la polisi Mkoani Simiyu linamshikilia Chigila Gilala mkazi wa kijiji cha Bukigi kata ya Malampaka wilayani Maswa (45) kwa kosa la kukutwa na viungo zinavyodhaniwa kuwa vya binadamu likiwemo fuvu la kichwa.

Mtuhumiwa huyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM katika kijiji hicho na Mganga wa tiba asili alikamatwa nyumbani kwake, baada ya kuwepo kwa taarifa kuwa- alikuwa amewahifadhi majambazi kwa ajili kugangwa (kuzindikwa).

Akitoa taarifa kwa waandishi wa kamanda wa -jeshi la polisi Mkoani Simiyu Gemini Mushy alieleza kuwa tukio hilo la kukamatwa kwa mwenyekiti huyo lilitokea Mei 9 mwaka huu -majira ya saa 11 jioni katika kijiji hicho.

Kamanda Mushy alisema kuwa askari wakiongozwa na mkuu wa upelelezi katika wilaya ya Maswa walipata taarifa kutoka kwa raia wema kuwepo kwa majambazi nyumbani kwa mganga huyo, kuwa alikuwa amewahifadhi kwa ajili ya kuwazindika.

Alisema baada ya kupata taarifa hizo walifanya msako nyumbani kwa mwenyekiti huyo, ambapo- alibainisha kuwa walianza kufanya upekuzi ndani na nje ya nyumba.

“Wakati wakifanya upekuzi huo walikutana na mfuko wa sandarusi ukiwa chini ya lundo la kuni nje ya nyumba- ya mwenyekiti huyo..na katika mfuko huo kulipatikana fuvu la kichwa pamoja na mifupa ya mikono au miguu vinavyodhaniwa kuwa ni viungo vya binadamu” Alisema Mushy.

Kamanda alieleza kuwa jeshi hilo linaendelea kufanya uchunguzi kama kweli viungo hivyo ni vya binadamu na kama anahusika na uwepo wa viungo hivyo kutokana na -kukutwa nje ya nyumba yake.

Wakati huo huo kamanda Mushy alibainisha kuwa jeshi hilo linamshikilia- Gandula Mashimo mkazi wa kijiji cha Longalombogo kata ya Migato wilaya ya Itilima Mkoani hapa kwa kukutwa na Bunduki ya kivita SMG na risasi 273.

Alisema kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa juzi majira ya saa 3:30 usiku kijijini hapo, akiwa embeba siraha hiyo pamoja na risasi katika mfuko wa sandarusi.

Alisema mtuhumiwa alikamatwa baada ya wananchi kutoa taarifa kwa jeshi la polisi wilayani humo, ambapo alikamatwa akiwa njiani kuelekea kusikojulikana.

Mushy alieleza kuwa uchunguzi unaendelea ili kubaini washirika wake, ikiwemo na matumizi ya silaha hiyo, huku akitoa wito kwa wananchi mkoani hapa kutoa taarifa za watu wanaowahisi kuwa siyo wema katika maeneo yao.

Aidha alitoa onyo kwa ambaye anamiliki silaha bila kibali rasmi, kuwa ajisalimishe pamoja na silaha yake mara moja kabla ya msako mkali kuanza.


Read More

Mchepuko wa Dingi Hautaki Tuachane...umenipa Mambo Matamu Sijawahi Pewa toka Nianze Mapenzi..

Leave a Comment
Nimekamatwa katikati ya penzi zito la mchepuko wa dingi yangu, Ipo hivi mimi nimeoa kwa miaka miwili sasa naishi Mwanza

wazazi wangu pia wanaishi hapa hapa Mwanza kwa takribani mwaka na kitu. Wamekua kwenye mgogoro mzito sana kuhusu huo mchepuko ambapo mzee kwa sasa anarudi home once in a week, siku zilizobaki zote analala kwa huo mchepuko ambao ameupangisha nyumba ya gharama kubwa na thamani za ndani pia.
Kwa kweli kachanganyikiwa vibaya juu ya huo mchepuko yaani ingekua bado tuna mhitaji kifedha labda bado tupo shule na kadhalika sieleewi ingekuaje. Cha kushukuru mungu wote tunafamilia zetu sasa hivi juzi kati kama miezi mitatu hivi dingi aliniuliza hivi ni lini utamfahamu mama yako mdogo maana wewe ndio mtoto wangu pekee wa kiume, nikamwambia mzee ni wewe tu, ukiwa tayari nipeleke dada zangu wote waligombana na mzee hivyo hawaongei kisa ni ugomvi wa wazazi kuhusu huo mchepuko hadi mama alipata ugonjwa wa hypertension juu ya huo mchepuko.

Nikapelekwa kuuona huo mchepuko, ila yy mwenyewe anatumia jina mama mdogo, kufika pale mtoto ni mkali sijaona, ni mweupeee utadhani Mwarabu, kiuno chembamba halafu wowowo hilo, kapiga kigauni hicho paja zote nje nikaambiwa mwamkie mamdogo huku umri anaonekana kulingana na mdogo wetu wa mwisho ambae pia ameolewa. Akamwambia binti hili ndo jembe langu peaneni namba za simu maana ikitokea nimeanguka huku huyu ndo unampigia simu kumtaarifu maana mzee ana medical condition flani hivi anaishi kwa masharti.

Mara kwa mara tumekua na mawasiliano na yule binti kwa mambo mbali mbali nimezoea kwenda pale hata kama Mzee hayupo kumsalimia, maana binti hulaumu mbona huji hata kunitembelea n.k. One day Mmee alikua nje ya Mwanza akanitumia list ya vitu nivinunue nimpelekee yule binti huwa hataki kabisa atoke. Nilipofika akatoa pombe kali akanipa yeye akawa anakunywa Dompo sikuwahi kunywa pombe kabla. Muda ulivyozidi kwenda tukaanza michezo ya kilevi, mara kuvutana na kadhalika kuja kustuka tupo dunia nyingine.

Nilishangaa ananivua nguo kama ugomvi vile mwisho tukawa tumeoana kwenye kochi pale.Nikiri tu wazi tangu kufahamu mapenzi mazito kama yale, kiuno kinazungushwa huwezi kama pana mfupa pale. Tuliendelea kufanya mchezo huo mara kwa mara, wakati mwingine natoroka kazini mchana naenda.Kwa kweli hata mke wangu anaachwa mbali sana na huyu binti kwa mambo hayo. Hata kabaang ambayo sikuwahi kufanya ndo nilipata for first time ni tamu mno nililia kama mtoto mdogo.

Hivi sasa nataka kujinasua nimeona naelekea kubaya, maana wife ameona mwenendo wangu umebadilika kwa hiii miezi mitatu ingawa mzee hana habari. Ila binti ndo amekua msumbufu hataki tufike mwisho. Mimi conscious ndo inanishtaki hasa kwa wife.Hata kwenda kwenye ibada nimeacha kwenda ikifika jumapili natafuta kisingizio chochote ili nisiende kwa sababu naona nafanya kazi bure kwa dhambi ya uzinzi na pombe ambavyo vyote nilikua sivifanyi kabla. Nimekuja kwenu mnisaidie nawezaje kuacha. Maana hata mzee akijua itakua balaa maana alishasema anataka kumuoa bomani

Naombeni msaada jamani
Read More

Lulu Ataja Sababu ya Kupenda Kutoka na Wanaume Waliomzidi Umri

Leave a Comment
Staa wa Filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amekili kupenda kuwa na mahusiano wa kimapenzi na wanaume waliomzidi umri.

Lulu Alizungumza hayo wakati akihojiwa kwenye kipindi cha 'The Sporah Show', Lulu amezitaja sababu za kupendelea kutoka na wanaume waliomzidi umri.
SPORAH: Watu wanahisi kwamba Lulu anapenda sana kutembea na watu waliomzidi umri sana.

LULU: That’s true, sio uongo, sio sana, Napenda kudate mtu ambaye anayeweza kusimama kama mpenzi, kama kaka, kama baba, kama kiongozi. Sitakuwa tayari kuwa na ile relation leo tumeamka na Maisha Club, kesho tumeamka na Billicanas, kesho tumeamka pale tunakula chips, I need to gain from you, nje ya upenzi unanifundisha nini kwa sababu haimaanishi kwamba mi ntaishi na wewe milele, itafikia siku labda we utaondoka au mi ntaondoka, we ukiondoka mi nikibaki nimejifunza nini kutoka kwako na ntaendelea kuishi vipi.”

“Haimaanishi kwamba napenda kutembea na watu walionizidi umri labda miaka hamsini, napenda kuwa na mtu ambaye angalau ananizidi umri, anauzoefu zaidi yangu, amepitia vitu vingi, anajua vitu vingi kwamba i’ll be there as a girlfriend lakini nakuwa naiba iba kidogo […] na vitu vingine vya kitoto kitoto vingi vinakuwa hamna.” alisema Lulu.
Read More

Kajala Apata nafuu Baada ya Kupigwa Chupa

Leave a Comment
Staa wa filamu za kibongo, Kajala Masanja anaendelea vizuri baada yakupigwa chupa na kijana mmoja usiku ya kuamkia jana wakiwa kwenye show ya mwanamziki Mabeste aliyoiandaa ili kuchangisha pesa kwa ajili ajili ya matibabu ya Mkeo.

Leo kupitia ukurasa wake mtandaoni, kajala ameweka picha hiyo hapo juu na kuandika “Maisha yanaendelea au sio......” kuonyesha kuwa yupo poa na anaendelea na masiha yake yakawida.

Akilezea tukio hilo la kupigwa na chupa hapo jana alipofanya mahojiano na mtangazaji Millard Ayo kajala alieleza kuwa

“Mpaka tumemaliza show, sasa kwenye muda wa kuondoka nikamwambia Meneja wangu amuite msanii wetu mmoja anaitwa Tausi ili tuondoke, sasa wakati nataka kushuka kwenye gari natembea tu sijui chochote nikashangaa chupa imenipiga usoni, nikadondoka na kubiringita kwenye zile ngazi, kuna mkaka na mdada wakaniona wakanisaidia”

Akaongeza kuwa;

“Aliyenipiga na hiyo chupa ni Mwanaume, simjui na wala sijawahi kumuona hata mara moja…. amekamatwa yuko Osterbay Polisi, nilivyotoka Maisha Club nilipelekwa Hospitali Mwananyamala nimeshonwa usoni aliponiumiza, tukarudi Polisi nikaandika maelezo”.

Pole Kajala
Read More

Taarifa kamili kuhusu Kajala kupigwa chupa

Leave a Comment
 Kajala akionekana na jeraha juu ya jicho lake la  kushoto kwenye shindano la vipaji Kinondoni Dar es salaam.
May 10 2015 mwigizaji wa bongomovie Kajala alikwenda kumsupport msanii Mabeste ambaye alifanya show New Maisha Club kwa ajili ya kuchangisha pesa za kumsaidia mke wake kwenye matibabu.

Kajala anasema.... ‘Mpaka tumemaliza show, sasa kwenye muda wa kuondoka nikamwambia Meneja wangu amuite msanii wetu mmoja anaitwa Tausi ili tuondoke, sasa wakati nataka kushuka kwenye gani natembea tu sijui chochote nikashangaa chupa imenipiga usoni, nikadondoka na kubiringika kwenye zile ngazi, kuna mkaka na mdada wakaniona wakanisaidia’

Kajala...‘Aliyenipiga na hiyo chupa ni Mwanaume, simjui na wala sijawahi kumuona hata mara moja…. amekamatwa yuko Osterbay Polisi, nilivyotoka Maisha Club nilipelekwa Hospitali Mwananyamala nimeshonwa usoni aliponiumiza, tukarudi Polisi nikaandika maelezo;

Kwenye sentensi nyingine Kajala amesema ‘Huyu Mwanaume aliulizwa pale Polisi anasema eti ni Pombe, lakini mtu eti Pombe umeingizwa ndani saa moja tu unakumbuka kwamba ni pombe ndio imekufanya hivyo? sio kweli….. itakua tu alidhamiria yeye mwenyewe’

Read More

Taarifa kuhusu Picha Chafu za Shilole Akiwa Stejini nchini Ubelgiji

Leave a Comment
Haya ndiyo maelezo ya wawili hao kuhusiana na picha za mwanadada shilole zikimuonyesha wazi sehemu ya kifua chake wakati akiwa stejini anatumbuiza huko nchini Ubelgiji.
Show ni movement na uwezi mkataza mtu kupiga picha ukiwa kwa stage'na kuna nguo za show na nguo za kutoka out kikawaida'ukiruka ruka sana sidiria ni rahisi kuchomoka akina dada mnafaham na mtu yupo stejini anakua hajitambui kama nini kimetokea coz yupo stejin kwenye mood ya kazi na kila mtu ni binadamu na ndio mana wengine wanateleza kwa stage huyo paparazi aliopiga picha alifanikiwa kuzoom na kipata picha mbaya lakin katika hali ya kawaida na watu waliokua wakicheza nae hawakuweza kugundua lolote'na kiubinaadamu kama muhandishi wa habari hakupaswa kuchagua picha ambayo kaonekana vibaya mana naamini alipata picha nyingi nzuri tu za kupost ila aliamua tu kumchafua'So Mashabiki kumbukeni alikua yupo kazini hakupanga itokee ivyo na yote mradi atoe burudani nzuri kama mlivyomzoea''ambae hana upeo mdogo wa kufikiria ataongea shit ila kaa jiulize ingekutokea wewe ungesemaje? naomba mtusaidie kurepost hii habari tunawapenda sana

Nuh Mziwanda
Read More

Wema Sepetu ‘Amsapoti’ Ali Kiba

Leave a Comment
Baada ya hapo juzi Diamond Platnum kupitia ukurasa wake wa Instagram mtandaoni kutoa lawama juu ya uteuzi wa vipengele vya tuzo za muziki za Kilimanjaro Music Awards za mwaka huu na pia kueleza kuwa yeye hata hamasisha watu wampigia kura yapo kuwa ametajwa kuwania vipengere vingi zaidi kwenye tuzo hizo, hali ni tofauti kwa upande wa pili ambapo Staa wa Bongo Movies Wema Sepetu na team yake wamekuwa mstari wa mbele kumpigia debe Ali Kiba ili watu wampigia kura ili anyakuwe tuzo zote.

Kitendo cha Wema ambaye alikuwa ni mpezi wa Diamond kumsapoti Ali Kiba ambaye kwasasa inaonekana ndiye msanii mwenye ushindani (Kisanaa) na Diamond kimechukuliwa kwa mitazamo tofauti na mashabiki wa  mastaa hawa.

Team za mastaa hawa mtandaoni maarufu kama Team Mond, Team Kiba na Team Wema wamekua na mitazomo tofauti juu ya hiki anachokifanya Wema na hadi kufikia kutoleana lugha chafu wakati team Diamond wanaponda; huku team Kiba na Wema kuwa upande mmoja.

“Unapenda kiba wakati umetemwa na chibu alafu hukumbuki arusha umefukuzwa katika show ya kiba aibu huna kweli we mdada team platnamz hapa”-mtu mmoja alikomenti

Team Wema na Team Kiba wanamuunga mkono

“Halafu watu wengine viazi sana humu ndani kapostiwa King king king kiba mara ooooh chibu who is the Chibu by the way haaaaaaaaa. Acheni usechu kma ni diamond huko huko kwenu uhanithi hatutaki siye halaaaaa hata kama ajibebisha mwataka ajibebishe kwenu khaaaaa. Hebu legooooooo  Wematwende sawa. Vote for King baaaaanaaaa Ama niniiiiiiiii”-mmoja alikomenti

Wema Sepetu akiwa ndiye staa wa bongo mwenye followers wengi zaidi kwenye mtandao picha wa instagram (587,000 hadi sasa) amekuwa akiweka ‘posters’ za Ali Kiba na kuandika maneno ya kumsifia kama;

“Im thinking Eye candy.... Dats da right post...”

“Too much cuteness on this poster tho......”

“Im thinking Eye candy.... Dats da right post...”

“Campaign Inaendelea ama nene.... Such a cutie...!!! Like I said, either he gets it or nat, He still Fiiiiiiiiiiiiine....! Hihihihihi.... JustSayin...!!!”a
Read More

Picha za Sherehe ya Zari White Party iliyofanyika Usiku wa Jana

Leave a Comment
Tazama Picha Mbali Mbali za Sherehe ya Zari White Party iliyofanyika Usiku wa Jana




















Read More

Huyu ndio kigogo mpya anaye toka na jack wolper

Leave a Comment
Achana na kina pedeshee Mangi, Dallas na Gee Modal, kigogo mpya wa staa wa sinema za Kibongo, Jacqueline Wolper Massawe safari hii amenaswa laivu wakijiachia kwa raha zao.

Kwa mujibu wa chanzo, kigogo huyo ni mtu mwenye fedha zake aitwaye Jimmy Mgaya ambaye ni Mbongo mfanyabiashara aishie nchini Afrika Kusini ‘Sauz’.

Chanzo hicho kilishusha data kuwa jamaa huyo ndiye aliyempangia Wolper nyumba ya kifahari iliyopo ushuani Mbezi-Beach jijini Dar.Huku akirusha picha za kimahaba za wawili hao, sosi wetu huyo alisema kuwa Jimmy ni ‘mtu f’lani hivi amazing’ kwa sababu anakata mkwanja kinoma.

Chanzo hicho kilidai kwamba picha za wawili hao wakijiachia zilipigwa maskani kwa jamaa huyo huko Durban kwenye Jimbo la KwaZulu-Natal nchini Afrika Kusini.

Baada ya jitihada za kumsaka mwanaume huyo kugonga mwamba, Wolper alipigiwa simu na kusomewa mashitaka yake juu ya mwanaume huyo ambapo mbali na kukiri kumfahamu Jimmy, alikuwa na haya ya kusema:

“Ni kweli namfahamu Jimmy, nilikutana naye kwenye mizunguko yangu nje ya nchi. Si kweli kwamba ni bwana’ngu. Kuhusu picha, nilipiga naye kama rafiki tu na sioni kama ni picha mbaya.”

Hivi karibuni Wolper alikiri kuwa na mwanaume lakini akawa anaogopa kumwanika kwa kuogopa kuporwa na wasichana wa mjini hivyo inaaminika ndiye huyo Jimmy.
Read More
Previous PostOlder Posts Home