DIAMOND ANUSURIKA KUCHOMWA KISU

Leave a Comment
Katika hali isiyokuwa ya kawaida mkali anayekimbiza katika anga la muziki wa Kizazi Kipya Bongo, Nasibu Abdul ‘Diamond Platinumz’ amenusurika kuchomwa kisu baada ya kushuka kwenye gari na kujichanganya na mashabiki wake.

Tukio hilo la kutishia usalama wa staa huyo lilijiri Mitaa ya Ilala jijini Dar, Jumanne iliyopita, wakati akirejea nyumbani kutoka Afrika Kusini ‘Sauz’ alikokuwa ameweka historia mwishoni mwa wiki iliyopita.

Katika tukio hilo lililoshuhudiwa na wanahabari wetu, kufuatia umati mkubwa uwanjani hapo, polisi walilazimika kumkataza Diamond kuzungumza na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali waliofika ili kusikia neno kufuatia ushindi wake mkubwa ambao umeipeleka Tanzania katika ramani ya muziki barani Afrika.

Alipoanza kuondoka uwanjani hapo, mashabiki hao nao waliandamana naye kuelekea mjini.
Baada ya kuona hivyo, mwimbaji huyo wa Ngoma ya Mdogomdogo alifunua sehemu ya juu (roof) ya gari lake aina ya Toyota Prado hivyo kujitokeza, huku akiziinua juu tuzo zake tatu kwa wafuasi wake hao.


Jamaa huyo aliendelea na msafara huo katika Barabara ya Nyerere hadi alipofika Tazara, ambako msafara huo ulikata kushoto kuelekea Buguruni.Baadaye ulikata kulia kuingia katika barabara inayoelekea Kariakoo.

Msanii huyo mwenye jina kubwa Afrika, aliamua kushuka kwenye gari na kutembea kwa miguu kuwaunga mkono mashabiki wake.

Msafara huo ambao ulisindikizwa na mamia ya watu, wakiwemo waendesha bodaboda, baiskeli, magari na watembea kwa miguu, ulipoingia katika Mitaa ya Ilala, gazeti hili lilimshuhudia njemba mmoja akitafuta upenyo ili aweze kumfikia bila mafanikio, kwani kila alipojaribu kuwapita watu, alishindwa.


Katika harakati hizo, mtu huyo ambaye hakufahamika jina wala anakotoka, kisu chake alichokuwa amekichomeka kiunoni, kilionekana kuwa na makali tayari kwa matumizi.

Wakati umati ukizidi kuongezeka na walinzi wa msanii huyo wakiwa wanahangaika kuhakikisha usalama wa bosi wao unakuwepo, hatimaye polisi nao walibaini uwezekano wa kuwepo kwa hatari, hivyo wakalazimika kumwamuru kupanda kwenye difenda yao ili kumnusuru.

Wakati hali hiyo ikijitokeza, baadhi ya watu waliohojiwa walisema wana wasiwasi na wafuasi wa msanii mwingine nyota, Ali Kiba (Team Ali Kiba) kuwa nyuma ya tukio hilo pamoja na wale wa mpenzi wake wa zamani, Wema Isaac Sepetu.


“Unajua mashabiki wa wasanii hawa ni kama wana uadui, maana hii ni zaidi ya unazi, kwa vyovyote wale wa Kiba hawajafurahishwa na mafanikio ya Diamond, kama wangepata nafasi wangeweza kumdhuru,” alisema shabiki mmoja wa muziki wa kizazi kipya, aliyejitambulisha kwa jina la Zepha.

“Usije ukashangaa hata mashabiki wa Wema nao wanaweza kuwa nyuma ya jambo hili. Mafanikio ya Diamond katika tuzo hizo ni kama msumari wa moto kwao, wanaweza kujiona kama wana mikosi, huenda ndiyo maana hapo mwanzo hakuweza kushinda tuzo zingine alizoshiriki nje ya nchi,” alisema shabiki mwingine wa muziki ambaye alikataa kujitambulisha.

Alipoulizwa Diamond hakuwa na la kusema juu ya ishu hiyo zaidi ya kuwashukuru mashabiki wake waliompokea.

“Nawashuru kwa kuendelea kunisapoti. Wameonesha wanapenda mafanikio ya msanii wao,” alisema Diamond anayedaiwa kuwa ‘klozi’ na mrembo Zari mwenye maskani yake Uganda na Sauz.
Next PostNewer Post Previous PostOlder Post Home

0 comments:

Post a Comment